TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya
ziara ya kushitukiza katika Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ambapo pamoja
na mambo mengine ameiagiza Benki hiyo kusitisha mara moja ulipaji wa
malimbikizo ya malipo ambayo tayari yalishaidhinishwa (Ex-Checker) na
badala yake yarejeshwe Wizara ya fedha na Mipango kwa ajili ya kufanyiwa
uhakiki.