Jumatano, 2 Septemba 2015

Jumanne, 1 Septemba 2015

LIVE UPDATE Kutoka Serena Hotel Ambako Dr. Slaa Anaongea


1.Napenda  kumshukuru  mwenyezi  mungu  kwa  kutujalia  uzima.

2. Nimeamua  kujitokeza  leo  hii  ili  kukomesha  upotoshaji  na  kuuweka  wazi  ukweli.


3.Sina  tabia  ya  kuyumbishwa  na  ninasimamia  ninachokiamini.

4.Sina  ugomvi  na  kiongozi  yeyote  maana  siasa  sio  uadui.

5. Siasa  inapoongozwa  kwa  misingi  ya  upotoshaji, matokeo  yake  ni  vurugu.

6. Naweka  wazi  kuwa  mimi  sikuwa  likizo  na  hakuna  mtu  yoyote  aliyenipa  likizo.

7.Kilichotokea  ni  kuwa  niliamua  kuachana  na  siasa  tangu  tarehe  28.7.2015  saa  sita  usiku  baada  ya  kutoridhishwa  na  kilichokuwa  kinaendelea  ndani  ya  chama  changu.

Sheria ya Makosa ya Mtandao kuanza kutumika leo.



Serikali imewatoa hofu wananchi kuhusu Sheria ya Makosa ya Mtandao inayoanza kutumika rasmi leo kuwa haijatungwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu, bali kwa maslahi mapana ya taifa na kuleta maendeleo ya nchi, kujenga uchumi imara na kupambana na wahalifu.

Lowassa: Miaka 50 ya Kuteswa na CCM Imetosha......Watanzania Msiogope Kufanya Mabadiliko


Mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amesema mwaka huu ni wa mabadiliko ili kuiokoa nchi na madeni mengi ambayo yanasababisha uchumi kuyumba.

Magufuli Atikisa Songea......Aweka shada la maua kwenye Kaburi la Marehemu Kapteni John Komba


Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania  kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa majimaji mjini Songea jana ambapo mkutano huo ulihudhuriwa na maelfu ya wananchi mkoani humo.

 Akizungumza katika mkutano huo wakati akiomba kura Dr. John Pombe Magufuli aliwaambia wananchi hao kuwa  anataka kuijenga Tanzania mpya yenye viwanda vikubwa, vya kati na vya chini ili kuboresha uchumi wa nchi  na kuongeza ajira kwa vijana wa kitanzania na kuleta mabadiliko bora na siyo bora mabadiliko.
 
 Alisema pia serikali yake itaongeza kasi ya ujenzi wa barabara , Zahanati na Hospitali , kuongeza mafao ya wafanyakazi wa sekta mbalimbali ili kuongeza tija ya kazi , wanafunzi kusoma bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne nk.
 
 Alisema ataongeza zaidi  kasi yake katika utendaji  tofauti na alipokuwa  Waziri wa ujenzi kwani hapo awali alikuwa akiagizwa kama waziri na sasa  akichaguliwa na watanzania kuwa rais  yeye ndiye atakayeagiza na ole wake waziri atakayemteua asitekeleze maagizo yake atakiona cha moto.
 
 Dr John Pombe Magufuli pia alitembelea  na kuweka shada la maua  kwenye kaburi la Kada maarufu wa CCM marehemu Kapten John Damiano Komba ambaye alifariki  miezi kadhaa iliyopita jijini Dar es salaam katika hospitali ya jeshi Lugalo na kuzikwa nyumbani kwao huko Lituhi wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ???????????????????????????????????? Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania

Jumla ya Mara Iliyotazamwa