Jumanne, 4 Agosti 2015

YALIYOJIRI KWENYE MKUTANO MKUU WA CHADEMA ULIOFANYIKA LEO NA KUWAPITISHA MH. LOWASSA KUWA MGOMBEA URAIS WA TANZANI

 Mkutano Mkuu wa CHADEMA ulianza kwa kuimba nyimbo ya taifaShehe Rajabu Katimba akiomba Dua wakati wa mkutano mkuu wa CHADEMA uliofanyika leo 
Mchungaji Zakaria Kakobe akitoa neno la mungu wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
 Naibu katibu Mkuu Zanzibar Mh. Salum Mwalim akifungua mkutano wa Baraza kuu uliofanyika leo    Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mh. Freeman Mbowe akisoma hutuba katika mkutano mkuu wakati wa mkutano mkuu uliofanyika leo kwenye ukumbi wa mlimani City jijini Dar Makamu wa kwanza wa Urais Zanzibar Mh Maalimu Seifu akizungumza jambo ambapo alisema " Kwa uwezo wa Mwenyezi mungu tutaweza kuingoa CCM kwani watanzania wako tayari kuyafata mabadiliko.na pia Mpaka dakika hii sijapata barua ya Prof Ibrahim Lipumba kujiuzulu na mpaka jana saa 4 usiku nilikuwa nae na sikuona dalili zozote za kuonyesha kupishana na jambo hili kama jinsi ilivyoripotiwa na moja ya gazeti.Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi taifa ,James Mbatia wakati anazungumza aliwauliza wajumbe wa mkutano huo kwamba mbona Mkutano Mkuu huu hauna magari ya washawasha na mabomu, Hii ni dhahiri kuonyesha kuwa imani imetawala ndani ya Chadema pamoja na UKAWA kuelekea safari ya uchaguzi Mkuu. Mwenyekiti wa waalimu Mh. Graison Graison Mkoba wakati wa anazungumza kwenye mkutano mkuu wa chadema alisema " Niliambiwa na rafiki yangu mmoja afisa misitu kuwa ukiukata mti usiuzuei awache uporomokea kuelekea unapotaka hata kama unataka kupasua mbao ukiuzuia utakufa"Na " Unapochemsha maji ili kumkimbiza chura itachukuwa muda chura kukimbia mpaka joto lipande kwenye maji ndio chura aondoke" hayo ndio maneno ninayowaachia wajumbe wa Mkutano Mkuu CHADEMAJuma Duni Haji mgombea mwenza wa UKAWA kupitia CUF wakati anazungumza kwenye mkutano huo alisema "Nimechukua maamuzi magumu kama Mh Edward Lowassa ili Kuimarisha UKAWA."Mimi nimeanza siasa nikiwa form 2 mambo nilikuwa na afro shirazi party mambo yalivyobadilika na mm nikabadilika napata kustaajabu ninapomuona askari aliyotoka katika familia ya kimaskini anakabidhiwa silaha kuwalinda wananchi na badala yake anapiga mtoto wa kimaskini dhana ya kutafuta uhuru imepotea"Mgombea wa Urais alieteuliwa na chama hicho, Mh. Edward Lowassa akiwashukuru wananchama wa CHADEMA kwa kumpokea na kuonyesha upendo wao na kuwaahidi kuwa atayakabili majukumu makubwa waliyomkabidhi.
 Pia wakati anazungumza alisema "Niwaahidi kuwa tutafanya kampeni za kiistarabu sio kampeni za matusi na tutashinda kwa kishindo kikubwa. Niwaahidi watanzania kuwatumikia kwa hali namali na wategemee mabadiliko makubwa." Mgombea wa Urais alieteuliwa na chama hicho, Mh. Edward Lowassa akiwa kwenye picha ya pamoja na Mgombea Mwenza wake, Mh. Dkt. Juma Haji DuniMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe (wa pili kushoto) akiwa ameshikana mikono na Mgombea wa Urais alieteuliwa na chama hicho, Mh. Edward Lowassa (wa kwanza kushoto) pamoja na Mgombea Mwenza wake, Mh. Dkt. Juma Haji Duni (wa pili kutoka kulia) pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad (kulia), wakati wakitambulishwa kwenye Mkutano Mkuu wa Chama hicho, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

 Picha ya pamoja ya wenyeviti, wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wanachi (UKAWA) Makamu wenyeviti na Naibu Makatibu wakuuwa wa Cahadema wakiwa na mgombea urais Edward Lowassa na mgombea mwenza Haji Duni kwenye picha ya pamojaWananchama wakiwa ndani ya mkutano
 Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema Taifa, Halima Mdee


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa