Jumatano, 15 Julai 2015

MGOMBEA WA UKAWA KUTANGAZWA NDANI YA SIKU SABA


Mgombea urais ndani ya UKAWA kuja kutangazwa kwa shamrashamra ni ndani ya siku saba.

Ni baada ya kikao (summit) kukamilisha maridhiano ambapo kilizungumzia jinsi gani ya kuachina majimbo yalibaki na swala la mgombe urais

Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa NCCR Mageuzi JAMES MBATIA aliwaeleza wanahabari kuwa taratibu zote zimekamilika ndani ya vyama vinavyounda UKAWA na kilichobaki ni jinsi gani ya kumtangaza mgombea urais ndani ya UKAWA kwa kushirikiana na vyama vyote vinavyounda umoja huo, ndani ya siku saba .

Huku akiwasisitiza watanzania kuwa wavumilivu na kuwataka wajitokeze kujiandikisha katika daftari la kudumula wapiga kura linalotegemewa kuanza punde katika mkoa wa Dar es Salaam huku wakitega maskio yao na kumpokea mgombea urais ambaye atatambulishwa kuipeperusha bendera kupitia UKAWA.

Akijibu swali la mwandishi wa habari aliyeuliza swali
Je, ni kweli kama ilivyotapaka katika mitandao ya jamii juu ya Lowassa Kujiunga na chama kimojawapo ndani vyama vinavyounga UKAWA?

Akijibu swali hilo kwa kulitolea mifano ya mitandao ya jamii inayotumika na watu fulani kwa maswai yao binafsi na sio kuelimisha jamii, Mh Jamse Mbatia ilizungumzia moja ya account ya twitter iliyofunguliwa kwa jina mtandao mkubwa duniani BBC ikieleza kuwa Lowassa tayari ameshajiunga katika chama cha ACT na kusisitiza habari hizo sio za kweli huku akiwashauri watanzania kupima uzito wa habri na chombo kinachokiwasilisha na kuwataka wananchu wafatilie habari za vyama kupitia mitandao ya vyama.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa