Jumatatu, 13 Julai 2015

Urais 2015: Magufuli amteua makamu wa Rais Mwanamke


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuri mara baada ya kuteuliwa kuipeperusha Bendera ya Chama cha Mapinduzi(CCM) katika uchaguzi mkuu ujao amemteua Samia Suluhu Hassan kuwa makamu wake wa Rais endapo atashinda katika uchaguzi mkuu ujao.
 
Akizungumza kwa furaha katika ukumbi mpya wa  CCM uliopo hapa mkoani Dodoma Magufuli amesema alipoteuliwa kuwa Naibu waziri Samia alikuwa ndiye waziri wake hivyo yeye ndiye aliyemfundidha kufanya kazi na kupata ujasiri uliomfikisha hadi sasa anateuliwa kushika wadhfa mkubwa ndani ya chama cha Mapinduzi.
 
Magufuri  amewashukuru wajumbe kwa uteuzi huo na kuwa na imani naye huku akiwaahidi kuwa anaenda kutenda yale yote waliyo mtuma na kuahidi kuitekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2015-2020.
 
Ushindi huo wa Magufuli umepokelewa kwa shangwe na  wanasiasa takribani wa kambi zote zilizokuwa zinasigana na  kutishia kuleta mtifuano  ikiwemo baadhi ya wajumbe kutangaza kutokubaliana na maamuzi ya chama kwa uteuzi huo akiwemo Mbunge wa Songea Emmanuel Nchimbi.
 
Kwa upande wa wajumbe wanawake kutoka maeneo mbalimbali wamesema kuwa wana imani na Magufuli kwa kuwa ni mtu wa vitendo na sio wa maneno kama walivyo wanansiasa wengine.
 
Magufuli alichukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa ndani ya chama cha mapinduzi tarehe nne juni na kuacha gumzo kwa waandishi wa habari kufuatia kuwakacha  Waandishi waliokuwa wana msubiri pamoja na wanachama wa  chama cha Mapinduzi waliokuwa ukumbini wakimsubiri azungumzie vipaumbele vyake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa