Alhamisi, 4 Juni 2015

Fredrick Sumaye, Siyatemi wachukua fomu za kugombea urais


Waziri wa awamu ya Tatu Fredrick Sumaye akichukua fomu ya kugombea urais mwaka huu.
 

Waziri Mkuu mstaafu   wa  awamu ya Tatu Fredrick Sumaye pamoja na Amos Siyatemi  jana wamechukua fomu za kugombea urais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi makao makuu  ya CCM Mkoani  Dodoma .
 
Pazia la kuchukulia fomu lilifunguliwa na Amos  Siyatemi  majira ya nne akifuatiwa na Sumaye majira ya saa tano na nusu.
 
Akizungumza wakati wa kuchukua fomu  Sumaye  alisema moja ya kipaumbele chake ni kupamabana na rushwa, ufisadi   na  mauaji ya albino yanayoendelea nchini Tanzania hivisasa. 
 
Kipaumbelea  chake  kingine ni kukuza uchumi ili kukabiliana na wimbi la vijana wanao maliza vyuo vikuu pamoja na vyuo vingine.
 
Alisisitiza kuwa ataunda kitendo cha kuhujumu uchumi pamoja na kutenga kati ya wafanya biashara na watendaji wa serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa