Alhamisi, 4 Juni 2015

MAGUFULI NAYE HAKUWA MBALI KACHUKUA FOMU KUGOMBEA URAISI 2015 CCM.


Waziri wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuri akionesha fomu ya kugombea urais 2015
 
Waziri wa Ujenzi Dk. John Pombe Magufuri jana alichukua fomu  ya kugombea urais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi.
 
Akizungumza mara baada ya kupokea fomu ya kugombea Urais Magufuri alisema kwamba  hajui kwenye fomu hizo kimeandikwa nini hivyo kuomba muda zaidi wa kuzisoma na kuahidi kuwa atazungumza na Waandishi wa Habari muda ukifika.
 
Katika hatua nyingine Magufuri alisema kwamba moja ya kipaumbele chake ni kutekeleza ilani ya chama Cha Mapinduzi katika kitabu cha ilani  alichokishika  wakati akichukua fomu ya kugombea urais.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa