Ijumaa, 6 Februari 2015

BEYONCE AANZISHA BIASHARA YA CHAKULA MAALUM KWA DIET

 Mwanamuziki nyota wa miondoko ya Pop ulimwenguni Beyonce amekuja na biashara mpya inayohusisha chakula ambacho kinashauriwa na madaktari .
Beyonce ameungana na daktari mmoja anayefahamika kama Marco Borges ambaye ni mwanasaikolojia wa mazoezi na wawili hawa wamekuja na mpango wa kufanya biashara ya kupelekea watu vyakula vya mboga ambavyo vinashauriwa na madaktari
Aina ya chakula atakayouza beyonce itakwenda sambamba na mpangilio maalum wa kula unaomsaidia mtu kupungua uzito na kubakia katika uzito wa kawaida unaoshauriwa kiafya huku ukiwa na msaada mkubwa sana kwa watu wenye matatizo ya uzito .
Biashara hii imetokana na diet ambayo Jay na Beyonce waliifanya kwa muda wa siku 22 ambapo walikuwa wanakula vyakula vya mboga pekee.
Beyonce aliamua kuja na wazo hili la biashara baada ya kufuata mpangilio wa kula wa siku 22 ambao 

alifuata akiwa na mumewe Jay Z mpango ambao unasaidia kupungua uzito na kurutubisha mwili .
Jay Z alizungumzia mpangilio mpya wa chakula ambao yeye na mkewe wataufuata siku moja kabla ya siku yake ya kuzaliwa ambapo aliandika kwenye mtandao wa Life and Times kuwa siku moja kabla ya kufikia siku yake ya kuzaliwa akiwa anatimiza miaka 44 ataanza mpangilio mpya wa chakula ambao utahusisha vyakula vya mboga pekee.

Hata hivyo bado haijafahamika lini biashara hii ya chakula ya Beyonce na Marco Borges itaingia sokoni 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa