Ijumaa, 27 Machi 2015

CHAMA CHA WALIMU LUDEWA CHATOA TAMKO KALI LA KUPINGA KODI KATIKA NYUMBA WANAZOISHI WALIMU

Mwenyekiti mpya wa  chama cha walimu(CWT) wilaya ya Ludewa Mwalimu Fikiri Mgina akiwashukuru wajumbe kwa kumachagua kuwa kiongozi wao kwa muda wa miaka mitano ijayo.

Hii ndiyo safu mpya ya uongozi wa chama cha walimu wilaya ya Ludewa





Mhasibu wa Chama cha walimu wilaya ya Ludewa Bw.Mvanginyi



Chama cha walimu wilaya ya Ludewa (CWT) katika mkoa wa Njombe kimetoa tamko kali dhidi ya uongozi wa Halmashauri ya wilaya la kupinga kitendo cha walimu kukatwa hela katika mishahara yao kwaajili ya kulipia kodi za nyumba katika maeneo ya kazi.

Tamko hilo limetolewa na mwenyekiti mpya wa chama hicho Mwalimu Fikiri Mgina baada ya kumaliza uchaguzi wa vingozi wa  CWT ngazi ya wilaya ambapo aliitaka Halmashauri kutowatoza kodi walimu katika nyumba wanazoishi kutokana na walimu kufanya kazi katika mazingira magumu na kutokuwa na posho za muda waziada.

Mwalimu Mgina alisema kuwa ifike wakati Serikali itambue mchango wa walimu katika maendeleo ya Taifa na si kuwakandamiza walimu katika kuwatoza michango inayowaumiza kwani ingefaa nyumba hizo ambazo hazina hazi ya kuishi walimu ziwe kama motisha kwa walimu.

“Walimu tuko tayari kuishi chini ya miti na tukiendelea kufanya kazi kutokana na manyanyaso tunayoyapata kwani kutulipisha kodi za nyumba katika nyumba mbovu ni sawa na kutunyanyasa,kuna baadhi ya idara wanapata malipo ya ziada wakati wamuda wa kazi lakini sisi hatuna hilo hivyo nyumba tunazoishi zingekuwa kama motisha kwa walimu “,alisema Mwalimu Mgina.

Malalamiko yao ya walimu juu ya kutozwa kodi za nyumba wilayani Ludewa yamekuwa yakitolewa mara kwa mara huku uongozi wa Halmashauri umekuwa ukisema unalifanyia kazi ili kupunguza kero hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa