Jumanne, 10 Machi 2015

Meya wa Ilala awaaga watumishi sita wa afya wa Manispaa hiyo wanaoenda kuongeza ujuzi Korea kusini

Dk Iyyovngchan Ktm kutoka Shirika la Maendele la Korea (KOICA) akisisitiza jambo kwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wakati kwa kuagana na watumishi sita wa afya wa Manispaa hiyo waliopata nafasi ya kwenda kuongeza ujuzi nchini Korea Kusini chini ya ufadhiliwa KOICA kwa ajili ya kuboresha huduma katika hospitali itakayojengwa Chanika.Kulia kwa Dr Iyyovngchan ni Afisa kutoka KOICA Seongbeom Ktm na wengine ni watumishi wataokwenda Korea.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akipeana mkono wa kuagana na Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Chanika Dk Betha Sanga ambaye pamoja na watumishi wengine sita wa afya wa Manispaa hiyo wamepata udhamini wa Serikali ya Korea Kusini kupitia Shirika lake la Maendeleo KOICA kwenda kuongeza ujuzi nchini Korea Kusini kwa ajili ya kuboresha huduma katika hospitali itakayojengwa Chanika. Wengine ni Dk Agatha Shinyala na Dk Mary Machemba wa Amana Hospitali. Nyuma ya Meya ni Afisa kutoka KOICA Seongbeom Ktm.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akiagana na Afisa kutoka shirika la Maendeleo la Korea Kusini (KOICA) Seongbeom Ktm muda mfupi baada ya hafla ya kuwaaga watumishi sita wa wa afya wa Manispaa ya Ilala waliopata nafasi ya kenda kuongeza ujuzi nchini Korea Kusini chini ya ufadhiliwa KOICA kwa ajili ya kuboresha huduma katika hospitali takayojengwa Chanika. Kati kati ni Dk Iyyovngchan Ktm kutoka KOICA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa