Alhamisi, 22 Januari 2015

CHAMELEONE AFUNGUKA: DIAMOND HAJAOA, ZARI HAJAOLEWA KWANI TATIZO LIKO WAPI WAKIWA WAPENZI?


10422036_10205910264180703_4118755449661033438_n


Muimbaji wa Uganda, Jose Chameleone ameuzungumzia uhusiano kati ya Zari Ttale na Diamond Platnumz ambao kwa sasa umekuwa maarufu mno Afrika Mashariki.
Akizungumza na mtandao wa Kenya, Ghafla, Chameleone alisema haoni kama kuna tatizo kwa mastaa hao kuwa wapenzi. “Kama wanapenda, hakuna tatizo,” alisema muimbaji huyo wa Valu Valu.
“Diamond hajaoa na Zari pia hajaolewa. Kuwa na uhusiano wa zamani hakumzuii (Zari) kuwa na uhusiano mwingine.”
Kauli hiyo ya Diamond imekuja siku chache tu baada ya Diamond kutangaza kuwa yeye na Zari wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza.

Kwa upande mwingine alipoulizwa kuhusu Diamond kama msanii, Chameleone alisema: Ni msanii mzuri pia.

 Namba ya wasanii wazuri Afrika Mashariki inazidi kukua. Ndio maana muziki wetu umeanza kuchezwa Nigeria sababu nguvu ni kubwa kutoka Afrika Mashariki.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa