Ijumaa, 23 Januari 2015

YANGA NOMA SANA! TFF WATEKELEZA AGIZO KUMFUNGIA REFA TEOFILE

IMG_0086
Na Bertha Lumala
Yanga SC noma sana! Inachokisema TFF wanafuata na kutekeleza. Ndivyo unacyoweza kusema. Ulikumbuka tamko la jana la Yanga SC kuhusu kubaguliwa na kukabwa koo kwa mshambuliaji Amisi Tambwe na nyota wa Ruvu Shooting? Useme nini tena kwa tamko hili la leo la TFF! Tega sikio…Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemfungia refa Mohamed Teofile kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu baada ya “KUSHINDWA KUIMUDU MECHI YA YANGA SS DHIDI YA RUVU SHOOTING.”Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Salum Chama akiwa Mwanza leo jioni ameuthibitishia mtandao huu juu ya kufungiwa kwa Teofile kuchezesha mechi msimu huu.“Ni kweli tumemwondoa kwenye ratiba ya marefa wa msimu huu Mohamed Teofile kwa sababu hakuimudu mechi ya iliyopita ya Yanga dhidi ya Ruvu Shooting. Ni mwamuzi huyo tu ambaye tumemchukulia hatua hadi sasa,” amesema Chama.

Uamuzi huo umetoka ikiwa ni siku moja tu, tena saa chache baada ya uongozi wa Yanga SC kutoa tamko la kuishinikiza TFF kuwafungia marefa waliochezesha mechi na kuanika hadharani ripoti ya kamisaa wa mechi hiyo iliyomalizika kwa suluhu.
Katika mkutano na waandishi wa habari katika ofisi za Makao Makuu ya Yanga jijini jana mchana, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, Jerry Muro alitoa masharti manne kwa TFF kuchukua hatua kali dhidi ya wachezaji wa Ruvu Shooting, kuwafungia marefa na maofisa wa Ruvu Shooting pamoja na kutowapanga tena waamuzi husika katika mechi zinazohusisha kikosi cha Yanga.
Leo TFF imetekeleza agizo moja wapo bila hata kueleza kikao cha Kamati ya Waamuzi ya shirikisho kimekaa lini na wapi kupitisha kupitia mkanda wa video ya mechi na ripoti za marefa na kamishina wa mechi kabla ya kutoa maamuzi hayo.
Marefa Michael Mkongwa na Yussuph Sekile waliokuwa wasaidizi wa Teofile pamoja na Kenneth Mapunda aliyekuwa refa wa mezani Jumamosi hawajaadhibiwa na kamati ya Chama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa