Alhamisi, 22 Januari 2015

Mkutano wa hadhara viwanja vya Jimbo la Uzini Unguja.

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakielekea viwanja vya Mkutano wa hadhara kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana,  
Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana akipandisha bendera ya Mabalozi wa jimbo la Uzini Unguja baada ya kukabidhi bendera kwa mabalozi wote wa jimbo hilo zilizotolewa na Mbunge wa Uzini Mhe. Mohaamed Seif Khatib.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg. Vuai Ali Vuai akisisitiza jambo kwa wananchi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya tunduni Wilaya ya Kati Unguja.
Wanachama wa CCM wakifuatilia mkutano wa hadhara wakati Katibu Mkuu wa CCM akihutubia katika viwanja vya Tunduni Wilaya ya Kati Unguja jimbo la Uzini.
Mbunge wa jimbo la Uzini Unguja Mhe. Mohammed Seif Khatib akizungumza na Wananchi wa jimbo lake baada ya kupewa nafasi na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana kutowa maelezo ya kukamilisha ahadi kwa Wananchi wa jimbo lake.

Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Kati Unguja baada ya kumaliza ziara yake katika Wilaya hiyo kujionea utekelezaji wa Ilani ya Uchanguzi ya CCM na kutembelea miradi ya maendeleo katika Wilaya hiyo.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakishangilia katika viwanja vya mkutano wa hadhara katika jimbo la Uzini Unguja 


 Mmoja wa Kiongozi wa timu za Mpira katika jimbo la Uzini Unguja akipokea Seti ya Jezi kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrarnan Omar Kinana.
 Viongozi wa timu 38 za Jimbo la Uzini wakiwa na jezi waliokabidhiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abulrahaman Kinana zilizotolewa na Mbunge wa Uzini Mhe. Mohammed Seif Khatib.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana akiwa na kadi tano za Waliokuwa wanachama wa Chadema na kujiunga na Chama cha Mapinduzi katika jimbo la Uzini Unguja Zanzibar 
 Mwanachama mpya kutoka Chama cha CHADEMA Bi Fatma Kassim akizungumza baada ya kukabidhiwa Kadi ya CCM na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahan Kinana, akiwa jukwaani akitowa maelezo kwa Wananchi baada ya kukabidhiwa kadi katika viwanja vya Tunduni Jimbo la Unguja Zanzibar. 
 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahaman Kinana akimkabidhi Kadi Mwanachama Mpya wa CCM aliyejiunga kutoka Chama  upinzani.
 Vijana wa Chama cha Mapinduzi waliojiunga na CCM kutoka vyama vya Upinzani wakila kiapo cha Utii wa Chama baada ya kukabidhiwa kadi zao na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulraham Kinana.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahaman Omar Kinana akijumuika na Wanachapa wapya wa CCM waliojiunga na CCM na jumuiya za Chama hicho, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Tunduni jimbo la Uzini Unguja Zanziba

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa