Jumapili, 31 Mei 2015

STAA WA HOLLYWOOD DOLPH LUNDGRED AMKOJOLEA MWENZAKE KWENYE NDEGE...TAZAMA PICHA



Dolph Lundgred amemkojolea star mwenzie Methew Pritelard

January Makamba: Taifa liko njia panda, Wananchi Chagueni Kiongozi Atakayeleta Maendeleo


NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, amesema kwa sasa nchi ipo njia panda, hivyo kuna haja ya kutumia busara ili kuchagua kiongozi atakayeleta maendeleo.

CHADEMA Wamteua Godbless Lema kuwa Kamanda wa Operesheni ya Uandikishaji wa Daftari la Wapigakura


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Kaskazini, kimemchagua Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema, kama Kamanda wa Operesheni ya Uandikishaji wa Daftari la Wapigakura katika kanda hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 1, 2015


Gwajima: Asiyempenda Lowassa Akale Limao!!!


Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Askofu Josephati Gwajima amesema kwamba mwananchi  au mwanasiasa  yeyote asiyempenda Mbunge wa Monduli Edward Lowassa akale limao

NDIVYO ILIVYOKUWA JANA NDANI YA JIJI LA ARUSHA KATIKA MKUTANO WA LOWASA.....................

 Mtangaza nia ya kuwania Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono maelfu ya wananchi waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo, wakati wa kutangaza nia yake hiyo ya kuwania Urais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mtangaza nia ya kuwania Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono maelfu ya wananchi waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo, wakati wa kutangaza nia yake hiyo ya kuwania Urais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 

MAAJABU:ONA MWANAUME ALIVYOPANDIKIZIWA USO WA MTU MWINGINE BAADA YA USO WAKE KUARIBIKA NA KUWEKEWA SURA YA MTU ALIYEKUFA


Picha ikimwonyesha Norris kabla hajapata ajali, alivyopata ajali na baada ya kuwekewa uso mwingine wa marehemu
Ajali nyingi duniani zimekua zikisababisha vifo vya watu wengi huku zikiacha wengine wakiwa na ulemavu wa maisha ambao huwasababishia kupoteza mwelekeo wa maisha yao na kukata tamaa kabisa.

Jumamosi, 30 Mei 2015

Mbunge Ahoji ziara ya Obama Nchini


MBUNGE wa Viti Maalum, Amina Abdallah Amour (CUF) ameitaka Serikali kueleza imefaidikaje na ujio wa Rais wa Marekani, Barrack Obama mwaka 2013.
 

MOI Yaongoza kwa Upasuaji Kidunia


TAASISI ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) imetangazwa kitovu cha weledi duniani katika upasuaji wa mfupa mrefu wa paja na wa chini ya goti kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wenye mafanikio makubwa kuliko nchi nyingine yeyote duniani.

Wema Sepetu na Idris Nusura Wazichape


Malkia anayemiliki Kampuni ya Endless Fame Production, Wema Isaac Sepetu na Mshindi wa Big Brother Africa 2014/15, Idris Sultan ambao wamekuwa marafiki wakubwa katika siku za hivi karibuni, nusu wazichape kavukavu baada ya kupishana kauli huku wivu wa kimapenzi ukitajwa.

Ijumaa, 29 Mei 2015

Kina Mramba na Daniel Yona Kuhukumiwa Juni 30......Wanakabiliwa na Matumizi Mabaya ya Ofisi


HUKUMU ya kesi inayowakabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na wenzao inatarajiwa kusomwa Juni 30, mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Lowassa aitikisa Arusha......Watu wafurika, Wakosa vyumba Walala katika Magari, wengine wajiapiza Kulala Uwanjani....... Mkuu wa Majeshi mstaafu naye Atinga, fulana zenye Picha yake Zapanda Bei


NYUMBA za kulala wageni katika Jiji la Arusha na viunga vyake zimeanza kufurika kutokana na makundi ya watu yanayowasili jijini hapa kushuhudia mwanzo wa ‘Safari ya Matumaini’ ya Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa  Monduli Edward Lowasa, anayoianza rasmi leo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Tarehe 30 May 2015


Jumatano, 27 Mei 2015

TANZANIA KUTOA NAFASI ZAIDI KUWEZESHA WAKIMBIZI KUWA NA MAISHA YA KAWAIDA DSC_0009

DSC_0009
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe (kulia) akiwasili kwenye uwanja wa ndege Kigoma akiwa ameambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole (wa pili kulia) na kupokelewa na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Kigoma ambaye pia ni Katibu Tawala wa mkoa huo, Mhandisi Dkt. John Ndunguru (wa pili kushoto) kwa ajili ya kutembelea na kuona changamoto katika maeneo maalum wanapohifadhiwa Wakimbizi. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Juma Abdulla Saadala.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).

KALI YA MWAKA :SPIKA ANNA MAKINDA "AISIFIA" BANGI YA NJOMBE BUNGENI

Spika wa Bunge Anne Makinda amesema bangi inayolimwa katika Mkoa wa Njombe si kali kama inayolimwa Mikoa mingine kutokana na baridi kali iliyopo Mkoani humo.

NYERERE APEWA TUZO

Shehe wa mkoa wa mbeya  kulia Ndugu Mohamed Mwansansu pamoja na Askofu Thomas Kongolo mwakilishi wa jukwaa la wakristo mkoa wa mbeya kwa pamoja wakimkabidhi tuzo Mheshimiwa Makongoro Nyerere (Mb) afrika mashariki kwa niaba ya familia ya Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julias Nyerere tuzo ambayo imetolewa na viongozi hao wa dini kwa kutambua mchango na utumishi uliotukuka kwa Baba wa taifa mwalimu Nyerere , hafla ambayo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkapa jijini mbeya Mei 25 mwaka huu.

ALI KIBA NA JOKATE Penzi ni Kikohozi Uwezi Kulificha, Wathibitisha Uhusiano wao kwa Picha Hizi


Fresh Jumbe aliwahi kusema penzi ni kikohozi kulificha huwezi.
Na sasa penzi la Jokate Mwegelo na Alikiba limefikia hatua ambayo haliwezi kuwa siri tena. Wawili hao wamekuwa wakidaiwa kuwa wapenzi kwa miezi kadhaa sasa lakini bado binafsi hawajeza kukubali wala kukataa.

RAIS WA ZANZIBAR, DK. SHEIN AFUNGA MKUTANO WA MABALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JIJINI DAR

Balozi Seif kwa Niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein akiufunga Mkutano wa Nne wa siku Tatu wa Mabalozi wa Tanzania uliokuwa ukifanyika katika Hoteli ya Ramada Mjini Dar es Salaam.

Nyota Ya Lowassa Bado Inang'aa: Utafiti Mpya Waonyesha Anaongoza Kwa Kupendwa na Wapiga Kura Wengi......Wafuatia Slaa, Magufuli na Membe


Nyota ya Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, imeendelea kung’aa baada ya Taasisi ya Samunge Social Sciences Research Center (SSSRC), kufanya utafiti na kubaini kuwa kiongozi huyo ni chaguo la kwanza kwa wananchi.

Wizi TTCL Unatisha......Kambi Ya Upinzani Yaibua Tuhuma Nzito, Serikali Yabanwa Itoe Majibu


KAMBI Rasmi ya Upinzani bungeni, jana imeibua tuhuma nzito bungeni Mjini Dodoma dhidi ya Kampuni ya Simu nchini (TTCL), ikidai aliyekuwa Meneja Biashara wa kampuni hiyo (bila kutajwa jina), amefungua akaunti nchini yenye kiasi cha sh. bilioni moja.

UNYAMA Jijini Mwanza: Bibi Amchoma Visu Vya Moto Mjukuu Wake Akimtuhumu Kupoteza Peni Ya Sh. 200


Jeshi  la  Polisi  Mkoani  Mwanza  linamshikilia  bibi  mmoja  ajulikanaye   kwa  majina  ya  Laurencia  Athanas  mkazi  wa  Kiseke,

Jumanne, 26 Mei 2015

BVR Kigoma yalalamikiwa......Wananchi Walala Kituoni Kujiandikisha


Zoezi la uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa kielektoronik BVR umelalamikiwa na wananchi katika manispaa ya Kigoma Ujiji kutokana na kuchelewa kuandikishwa licha ya wananchi kulala kwa zaidi ya siku mbili katika vituo vya kuandikishia.

Mbio za Urais Za Benard Membe Zitaanzia Kijijini Kwake......Asema Wakati Ukifika Atachukua FOMU.


Siku mbili baada makada waliokuwa wamefungiwa kwa makosa ya kukiuka kanuni za CCM kuachiwa huru, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ameeleza nia yake kuwa wakati ukifika atachukua fomu kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

K-Lynn azungumzia maisha yake kama mama, kwanini hawezi kurudi kwenye muziki na kazi ya interior design


Ni nadra sana kukutana na Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi maarufu kama K-Lynn lakini kupitia tuzo za watu tulifanikiwa kupiga story mbili tatu.

Filamu ya Van Vicker na Wema Sepetu ‘Day After Death’ kuzinduliwa September, Dar


Filamu ya Wema Sepetu na muigizaji wa Ghana, Van Vicker ‘Day After Death’ inatarajiwa kuzinduliwa September mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Maelezo Ya KINA Ya Edward Lowassa Kuhusiana Na Sakata La Richmond, Afya Yake, Utajiri Wake Na Kwa Nini Alikuwa Kimya Kwa Miaka Yote 7


Hatimaye  Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana alivunja ukimya wa muda mrefu alipofanya mahojiano ya ana kwa ana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari.

Jumatano, 20 Mei 2015

Wanafunzi wa chuo kikuu cha UDSM wagoma kuingia darasani kwa madai ya kutopewa fedha za kujikimu.


Maelfu ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani wameanza mgomo kuingia darasani kwa madai ya kutopewa fedha za kujikimu kwa zaidi ya wiki 11 huku wakitaja gharama za maisha zikiwa zimepanda mara dufu.

Kipindupindu Chalipuka kwa wakimbizi wa Burundi Walioko Katika Kambi ya Kigoma.


WAKATI hali ya usalama nchini Burundi ikiwa bado tete, wakimbizi 558 walioko katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma wanaugua ugonjwa wa Kipindupindu.

Jumatatu, 11 Mei 2015

Wanafunzi 'WAPIGWA' Mkutano Ukawa Arusha


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, wanafunzi wa shule za msingi za Mwangaza na Ngarenaro, juzi walidaiwa kupata kipigo kutoka kwa vijana waliojiita ‘Makamanda’ wa umoja wa vyama vya siasa vya upinzani ujulikanao kama Ukawa, baada ya baadhi yao kufika katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya karibu na shule yao.

Jumapili, 10 Mei 2015

Mganga akutwa akiroga mahakamani


MGANGA mmoja wa kienyeji amekamatwa akifanya ushirikina katika Mahakama ya wilaya ya Bunda mkoani Mara kwa kutumia tunguli ili kuwezesha kushinda kesi.

Pinda: Tumedhamiria kuitokomeza malaria


WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la ugonjwa wa malaria kwa kuamua kujenga kiwanda cha kisasa cha kutengeneza dawa za kuua viluwiluwi wa mbu wanaosababisha ugonjwa huo.

Laizer ajitokeza kupambana na Lema


JOTO la ubunge kwenye jimbo la Arusha Mjini, limezidi kupanda mara baada ya kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Arusha, Francis Laizer kutangaza rasmi kuwania ubunge katika jimbo hilo, endapo akipewa ridhaa na chama chake kugombea.

Maandamano Burundi yachukua sura mpya


Serikali ya Burundi imewataka  waandamanaji katika mji mkuu wa Burundi Bujumbura kusitisha maandamano yao dhidi ya hatua ya rais wa taifa hilo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu katika uchaguzi wa mwezi ujao.

Kenya wamtaka Rais Kikwete kuingilia kati mgogoro Burundi


Wananchi  nchini Kenya wamemtaka mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambaye ni Rais wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete kuingilia kati mgogoro wa Burundi uliopelekea wanachi zaidi  ya kumi kufariki dunia na wengine kukimbilia nchini Tanzania.

Diwani CUF Mbaroni kwa Tuhuma za Kuomba na Kupokea Rushwa ya Sh 150,000


DIWANI wa Kata ya Ngula wilayani Kwimba, Palu Mashagu (CUF), anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh 150,000.

FILIKUNJOMBE AWEKA HISTORIA LUDEWA

Filikunjombe akikabidhi kitanda cha kujifungulia akina mama katika kijiji cha Lupanga
Filikunjombe akikabidhi kitanda cha kujifungulia katika kijiji cha Mavanga

Jumamosi, 9 Mei 2015

Mgawanyo Wa Majimbo UKAWA: CHADEMA Yaachiwa Jimbo Moja Zanzibar


UMOJA wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umeridhia Chama cha Wananchi (CUF) kusimamisha wagombea wake wa nafasi ya ubunge katika majimbo yote ya uchaguzi visiwani Zanzibar, isipokuwa katika Jimbo la Kikwajuni.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana Makao Makuu ya CUF, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa CUF, Omar Ali Sheikh, alisema Ukawa wamekubaliana katika Jimbo la Kikwajuni watasimamisha mgombea ubunge kutoka Chadema ambaye ni Salum Mwalimu.
 
Mwalimu ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), ambaye hata hivyo tangu ateuliwe amekuwa akifanya kazi zake Tanzania Bara.
Jimbo la Kikwajuni linaunganisha wakazi wa maeneo ya Kikwajuni Juu na Chini, Kisimamajongoo, Kilimani, Miembeni, Magereza na sehemu ya eneo la Michenzani.
 
Uamuzi wa Mwalimu kusimama kuwania ubunge Jimbo la Kikwajuni kupitia Chadema, umepokewa kwa hisia tofauti miongoni mwa wachambuzi wa siasa ndani ya jimbo hilo huku wakionesha uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 30 huenda utaleta changamoto kubwa kwa CCM.
 
Changamoto kubwa inayoonekana kwa CCM ni kwamba, Mwalimu amezaliwa na anatoka katika familia yenye makazi katika eneo maarufu la Kisimamajongoo ambalo lilikuwa ni kitovu cha harakati za siasa za Chama cha Afro Shiraz (ASP).
 
Wachambuzi wanasema kwa namna moja ama nyingine familia ya Mwalimu nayo ilishiriki kinagaubaga katika harakati za kudai ukombozi kwa Mzanzibari zilizofanywa na hayati Mzee Karume.
 
Eneo la Kisimamajongoo ndilo lilikuwa kitovu cha harakati za ASP kudai uhuru wa Mzanzibari kutoka kwa Sultani na Wanamapinduzi walikuwa wakikutana katika eneo hilo kupanga mikakati yao wakiongozwa na hayati Mzee Karume katika nyumba yake aliyoipa jina la ‘Ndiyo’.
 
Hata hivyo, zilipokuja siasa za ushindani, baadhi ya wakazi wake wakagawanyika na kujiunga na Chama cha Wananchi (CUF).
 
Wakazi wa eneo la Kisimamajongoo wanaaminika ni ndugu wa damu na hilo ndilo linasemwa huenda likawa ni moja ya jambo litakalowavutia wananchi wa jimbo hilo kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kuamua kumpa uongozi Mwalimu wakiamini ni kijana wao na hatowaangusha.
 
Mwalimu licha ya kuwa amezaliwa katika eneo la Kisimamajongoo, lakini wachambuzi wanasema pia katika uchaguzi huo atabebwa sana na umaarufu wa mama yake mzazi ambaye ni mtangazaji maarufu nchini, Faudhiyat Ismail Aboud.
 
Kwa sasa Jimbo la Kikwajuni kwa nafasi ya ubunge linaongozwa na Hamad Yussuf Massauni (CCM), ambaye pia ni mzaliwa wa eneo la Kisimamajongoo na hata katika uchaguzi wa mwaka 2010 alibebwa na turufu hiyo.
 
Inaaminika katika uchaguzi huo wananchi wote wa Jimbo la Kikwajuni kwa pamoja wakiongozwa na kampeni zilizofanywa na wakazi wa eneo la Kisimamajongoo, waliamua kumpa kura Hamad wakiamini kuwa ni kijana wao.
 
Wachambuzi wanasema uamuzi wa Ukawa kumsimamisha Salum Mwalimu, umefanywa kiutafiti zaidi wakiamini utaamsha ushindani mkubwa katika jimbo hilo ambalo limekuwa chini ya mikono ya CCM miaka yote.
 
Katika hatua nyingine, Mbunge wa Mji Mkongwe, Ibrahim Sanya, anatarajiwa kusimama tena kutetea nafasi yake katika uchaguzi ujao akichuana na Mwanahabari Maarufu, Ally Saleh ambaye ameshatangaza nia.
 
Katika nafasi ya Uwakilishi, CUF imemteua Ismail Jussa Ladhu kuwania nafasi hiyo akiwa ndiye mgombea pekee kutoka chama hicho.
 
Wakati huo huo, Mwandishi wetu kutoka Zanzibar, Is-haka Omar, anaripoti kuwa, CUF Zanzibar kimeeleza kuwa hatua yake ya kuendelea na mchakato wa uchaguzi ndani ya chama hicho katika majimbo 49 ya Zanzibar haiendi kinyume na makubaliano ya umoja huo.
 
Chama hicho kimesema hatua hiyo haitaathiri makubaliano kati ya vyama hivyo ya kuachiana majimbo katika uchaguzi mkuu ujao baada ya umoja huo kuridhia chama hicho kusimamisha wagombea katika nafasi zote za uchaguzi.
 
Pia CUF imesema jumla ya wanachama 327 wa chama hicho wamepitishwa kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge na uwakilishi wa majimbo na katika viti maalumu vya wanawake Zanzibar.
 
Kati ya wanachama hao, 133 wameteuliwa kugombea ubunge, 134 uwakilishi katika majimbo 49 huku wengine 29 wameteuliwa kugombea ubunge kupitia viti maalumu sawa na wengine 30 walioteuliwa kugombea uwakilishi.
 
Wagombea hao watapigiwa kura na wajumbe wa mikutano mikuu ya majimbo na wilaya ili kupatikana kwa mgombea mmoja ambaye ataidhinishwa na kikao cha baraza kuu la chama hicho.

Katika hatua nyingine chama hicho kimeendelea kusisitiza kuitaka ofisi ya vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi kuwapatia wananchi vitambulisho hivyo kabla ya kuanza kwa uandikishaji wa duru la mwisho unaotarajiwa kuanza wiki ijayo katika Jimbo la Micheweni ili kuepuka vurugu.

Bilioni 8 Kutumika Kupanga Upya Jiji la Mwanza


SERIKALI inakusudia kutumia Sh bilioni nane katika mpango wake wa kulipanga upya Jiji la Mwanza kwa kuainisha sehemu za makazi, viwanda, biashara na huduma za kijamii.

Hatima ya Lowassa, Membe sasa Mei 20


Filimbi ya kuanzisha mbio za urais kwa tiketi ya CCM itapulizwa Mei 23 baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho tawala, huku makada sita walio ‘kifungoni’ wakitarajia kujua hatima yao kwenye mbio hizo Mei 20. 

Jumatano, 6 Mei 2015

MPANGO WA FILIKUNJOMBE WILAYANI LUDEWA WAFANIKIWA.

Deo Filikunjombe akiongea na wananchi wa kijiji cha Mavanga
Filikunjombe akifurahi kwa kupinga ngoma na wanafunzi wa shule ya msingi Mavanga

Jumla ya Mara Iliyotazamwa