Jumatano, 27 Mei 2015

KALI YA MWAKA :SPIKA ANNA MAKINDA "AISIFIA" BANGI YA NJOMBE BUNGENI

Spika wa Bunge Anne Makinda amesema bangi inayolimwa katika Mkoa wa Njombe si kali kama inayolimwa Mikoa mingine kutokana na baridi kali iliyopo Mkoani humo.
Makinda alijikuta akitoa jibu hilo huku akicheka kutokana na swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa viti maalum Christowaja Mtinda ambaye alisema kuna maeneo nchini ukiwemo Mkoa wa Njombe mmea wa Bangi umekua ukiota bila kupandwa na hutumika kama chakula.
“Njombe bangi haioti yenyewe, tulikuwa tunapanda, lakini hata hivyo bangi ya njombe si kali kwa sababu ya baridi” Makinda.
Akijibu kwa niaba ya Waziri wa afya, Juma Nkamia alisema Serikali haipo tayari kuhalalisha matumizi ya bangi kama dawa kwa sababu athari zake ni nyingi kuliko faida.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa