Jumatatu, 4 Mei 2015

Mgomo Wa Daladala Waleta Shida Jijini Dar


Mgomo wa wafanyakazi wa mabasi yanayotoa huduma jijini Dar es Salaam, leo asubuhi umesababisha mtafaruku mkubwa kwa wakazi wa jiji hili ambapo wengi wao walionekana wakitembea kwa miguu kuelekea kazini na katika shughuli zao mbalimbali.
 
Mgomo huo ambao unaenda sambamba na usafiri wa mabasi ya abiria nchi nzima, unafuatia ule uliotokea Aprili 11 mwaka huu, ambapo wenye mabasi na wafanyakazi wanataka maridhiano na serikali katika masuala mbalimbali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa