Alhamisi, 9 Aprili 2015

Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) Chasema Mgomo wa Madereva Kesho ni Batili.....Kimesema Wamiliki Hawataki Magari Yao Yatumike Kuwagombanisha Na Serikali



Chama  cha  wamiliki  wa  mabasi  Tanzania, TABOA  kimesema  mgomo  wa  madereva  unaotarajiwa  kuanza  kesho  ni  batili.

Sababu  kubwa  ya  madereva  hao  kugoma  ni  kuishinikiza  serikali  kuweka  mfumo  mzuri  wa  ajira  na  kupinga  kanuni  inayowataka  kurudia  kusoma  katika  chuo  cha  taifa  cha  usafirishaji,NIT  kila  leseni  zao  zinapokwisha  muda.

Kwa  mujibu  wa  TABOA, madereva  waliopanga  kugoma  hawatambuliwi  kisheria,kwani  wapo  waliofukuzwa  kazi  kutokana  na  sababu  mbalimbali  ikwamo  kusababisha  ajali  na  sasa  hawana  magari  ya  kuendesha.

Mwenyekiti  wa  TABOA  Mkoa  wa  Dae  es  Salaam, Hamza  Mringo  alisema  madereva  wanaotambuliwa  kihalali  na  mamlaka  ya  usafirishaji  Nchi  kavu  na  majini,SUMATRA  hawajawahi  kushiriki  mgomo  uliofanyika  April mosi,  na  hawatashiriki  kamwe.

"Madereva  wetu  hawawezi  kugoma  kwa  sababu  tunaamini  kila  kitu  kinaamriwa  kwa  utaratibu,tumepanga  kukutana  na  serikali  tuone  jinsi  ya  utekelezaji  wa  hiyo  kanuni  inayoleta  shida.

"Baada  ya  kuongea  na  serikali  tukaelewana,tutakuwa  tayari  kuwalipia  madereva  wetu  kozi  ambazo  wao  wanaziona  ni  kero...inaelekea  mgomo  huu  unamkono  wa  mwanasiasa  mmoja  tunamjua," alisema.

"Wao  wana ajenda  yao  ya  siri,sisi  hatutaki  magari  yetu  yatumike  kama  ngao  ya  kutugombanisha  na  serikali.

"Mbaya  zaidi  hizi  vurugu  zao  wanataka  kuzifanyia  eneo  letu  la  kazi  ambalo  tumekabidhiwa  kihalali." Alisema

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa