Alhamisi, 16 Aprili 2015

Uzito wa hawa watoto ni tatizo, baba kaona afanye maamuzi magumu kuwaokoa !!

bonge msosi 
Baba mmoja India amefikia uamuzi wa kuuza figo yake ili kupata pesa za matibabu ya watoto wake ambao wana tatizo la kuwa na uzito mkubwa.
bonge1 
Watoto hao ambao wa kwanza ana miaka mitano uzito wake ni kg.48, wa pili anamiaka mitatu uzito wake ni kg. 34 na wa mwisho ana miezi 18 na uzito wake ni kg. 15, ni miongoni mwa watoto walioweka historia duniani kutokana na kuwa na uzito mkubwa.

bonge famil 
Wazazi wao wamesema wamekuwa wakipata wakati mgumu wa kuwahudumia watoto hao chakula kutokana na kula chakula kingi, kwa wiki wanakula chakula kinachotosha kuliwa na familia mbili kwa mwezi mzima.
bonge msosi 
Baba huyo ana hofu kuwa kama watoto wake wataendelea na hali hiyo huenda wakapoteza maisha kwa siku za baadaye, kaona atafute mteja wa kumuuzia figo yake moja ili apate hela kuwapeleka watoto hao kwa mtaalamu atakayewasaidia.
toto
Kwa siku watoto hao wawili Yogita na Anisha kawaida wanakula chapati 18, wali kilo tatu, mifuko sita ya crips, maboksi matano ya biskuti na ndizi 12.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter, instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>>twitter Insta Facebook

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa