Alhamisi, 30 Aprili 2015

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamuduni na Michezo, Dk. Fennela Mukangara Kuikabidhi Yanga kombe


WAZIRI wa Habari, Vijana Utamuduni na Michezo, Dk. Fennela Mukangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kukabidhi Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu Bara klabu ya Yanga, Mei 6 mwaka huu katika mchezo kati ya Azam FC dhidi ya timu hiyo.

Yanga imetwaa ubingwa huo Jumatatu hii ikiwa ni mara ya 25 tangu ilipoanza kushiriki ligi hiyo, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya timu ya Polisi Morogoro katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, huku ikiwa bado na michezo miwili mikononi kabla ya ligi hiyo kumalizika.

Baada ya mechi hiyo Yanga ilifikisha jumla ya pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine hata Azam ambao wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 45 na michezo miwili mkononi.

Yanga imewavua rasmi ubingwa huo Azam ambao ndio walikuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo ambalo walitwaa msimu uliopita.

Katika hatua nyingine Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji kufuatia timu yake kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu hiyo msimu wa 2014/2015.

Katika salamu zake, Malinzi amesema kutwaa Ubingwa wa VPL ni jambo muhimu na sasa wanapaswa kuanza maaandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa barani Afrika mwakani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa