Alhamisi, 9 Aprili 2015

RADIO ZA JAMII ZASHUKURU KWA KUPOKEA KATIBA INAYOPENDEKEZWA KWA NJIA YA SAUTI


akurugenzi na viongozi mbalimbali wa Radio za jamii wamethibitisha kupokea na kuanza kurusha Katiba Inayopendekezwa kwa njia ya sauti, makala na michezo ya radio iliyoandaliwa na Kampuni ya Focus Media na COMNETA zenye maudhui ya katiba inayopendekezwa.Wasimamizi wa redio za jamii wakisikiliza kwa makini wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

 Mwenyekiti wa Mtandao wa redio za Jamii, Joseph Sekiku akiongea machache kabla ya kuwagawia wasimamizi wa redio za jamii wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Wakizungumza na Focus Media ambao ndio waandaaji na wasambazaji wamekiri kwamba wamepokea kwa wakati muafaka, kwani hawakuwa na chanzo sahihi cha kupata maudhui yanayohusu elimu ya uraia na uchaguzi mkuu na kura ya maoni.

Baadhi ya wasimamizi wa radio zilizo katika mtandao wa radio za kijamii Community Media Network of Tanzania ambao wamethibitisha kupokea vitendea kazi hivyo ni Bw. Ali Khamis Mtwana, Mkurugenzi Mtendaji wa Tumbatu Island Community Radio, Bw. Anton Masai Triple A FM Arusha, Dr. Lazaro Ole Mongoi Mkurugenzi Mtendaji wa IDEA Radio, Henry Bernard, Adelina Lweramla, Jackson Mollel, wa ORS FM Arusha, Edwin Mpokasye, Radio Fadhila Mkurugenzi Radio Kwizera- Ngara.

Vipindi vinapokuwa vikiruka hewani wasikilizaji wamekuwa wakishiriki kwa kupiga simu na kuuliza maswali ilikuelewa zaidi Katiba Inayopendekezwa.

Wengine wanapiga simu kupongeza na mnamichezo ya radio ilivyoratibiwa vizuri na ikielimisha jamii juu ya mambo mbalimbali muhimu.

ILI KUSIKILIZA VIPINDI HIVI VYENYE MAUDHUI YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA TEMBELEA 

http://myradiostream.com/focusradiotz

www.katibainayopendekezwa.or.tz

www.facebook.com/KatibaInayopendekezwaTanzania


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa