Jumanne, 9 Desemba 2014

HALMASHAURI YA LUDEWA YAVUNJA MKATABA NA WANANCHI UJENZI WA MADUKA ,YAANZA KURUDISHA PESA ZAO ZAIDI YA TSH MILIONI 60

Baadhi ya  maduka  yaliyokuwa  yakijengwa  eneo la  uwanja  wa  mpira na mikutano wa mjini Ludewa ambayo kwa  sasa yamesitishwa  kujengwa  na halmashauri  kuanza  kurudisha  fidia kwa  kila mwenye jengo eneo hilo ambalo  awali  mkakaba  ulikuwa ni  wananchi kujenga na  kwa  kipindi  cha miaka mitano ya kuendesha  hao  wananchi hao  wangekuwa  wakilipa  nusu kodi na baada ya   kurudisha  gharama  zao  za  ujenzi  basi wangekuwa  ni  wapangaji kwa Halmashauri  hiyo

 Sehemu ya maduka  ambayo yalianzwa  kujengwa  hapo 

 Kutokana na  kuvunjwa kwa mkataba  huo  hivi  sasa  Halmashauri  itajengwa maduka  hayo kwa gharama  zake na  kukodisha kwa  bei  kulingana na  wakati  husika   ili  kukuza mapato ya  Halmashauri  hiyo ambayo kipato chake ni  chini  zaidi


 


HALMASHAURI ya  wilaya ya  Ludewa  mkoani  Njombe yaanzakurejesha fedha  zaidi  ya Tsh mlioni 68 kwa  wananchi  wake baada ya kuvunja mkakaba   kandamizi kwa  uchumi wa Halmashauri   huo kati yake na wananachi hao  baada ya  kubaini  kupata  hasara  kubwa zaidi .

Mkurugenzi  mtendaji  wa Halmashauri ya  wilaya ya  Ludewa Bw  Wiliam Waziri  ameueleza mtandao huu  wa matukiodaima  leo  kuwa hatua  ya kurejesha   fedha  hizo  ambazo ni kiasi cha Tsh milioni 3 kwa  kila mmiliki wa  jengo ene  hilo la  uwanja wa mpira na ule wa  mikutano mjini Ludewa baada ya  wananchi waliokuwa  wakijenga  hapo  kuonyesha  kugeuka makubaliano ya  mkataba .

Alisema  kuwa kwa  mujibu wa mkataba  wananchi hao  walipaswa  kujenga kwa gharama  zao  na kwa kipindi  cha miaka  mitano wangeweza  kurehjesha gharama  zao kwa  kulipa  kodi  ya  nusu  kodi na   nusu  ya   kodi   hiyo  kuweza  kuingia  katika mapato ya Halmashauri  na  baada ya  miaka  mitano ya  kurudisha gharama  zao basi wangeingia mkataba  upya kama  wapangaji  ambao  wangeanza  kulipa kodi  kulingana na viwango  pendekezi  vya kodi ya Halmashauri.

"Tumelazimika  kuvunja mkabata   huo   baada ya  kuona  wananchi  wameanza  kukiuka makubaliano mapema na iwapo  tutaacha hivyo  yawezekana Halmashauri  kukosa mapato  yake kama   ilivyo katika maduka ya  sokoni ambayo pia  mkataba   ulikuwa kama  huu ila baadae  waligeuka na  kulipa kodi ya Tsh 15000  kwa  mwaka "

Hivyo alisema  katika  kuepusha mapato  kuendelea  kukosekana katika Halmashauri  hiyo ambayo hadi  sasa haina  chanzo cha uhakika cha mapato  wamelazimika  kuvunja mkakaba   huo  na  kurejesha gharama  walizotumia kwa  kila mmoja na  kuzirejesha  ili zoezi la  kujenga maduka  hayo lifanywe na Halmashauri.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa