Jumamosi, 6 Desemba 2014

WAPOFUKA MACHO BAADA OPERATION


Maafisa wa utawala nchini Indiaa wanafanya uchunguzi kufuatia madai ya wagonjwa 15 kupofuka baada ya kufanyiwa upasuaji wa kutibu ugonjwa ujulikanao kama ''mtoto wa Macho' au Cataract bila malipo.


Upasuaji huo ulikuwa unafanywa na shirika moja lisilo la kiserikali katika kambi iliyotengewa matibabu hayo.

Maafisa wakuu wanasema kua kambi ambako upausuaji huo ulifanyika haikuwa na idhini inayostahili na pia waliokua wanaufanya upasuaji huo hawakuwa na vifaa vinavyostahili.

Lakini tajiri mmoja ambaye alifadhili mradhi huo, alisema wagonjwa wote 49 wa macho waliofanyiwa upasuaji walipewa huduma nzuri.

Mfumo wa afya nchini India uko chini ya darubini hasa baada ya wanawake 15 kufariki baada ya kufanyiwa upasuaji wa kufungwa kizazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa