Jumapili, 7 Desemba 2014

RAIA WA MAREKANI NA A.KUSINI

Raia wa marekani Luke Somers na mwenzak wa Afrika kusini Pierre Korkie wameuawa na wapiganaji wa kundi la Alqaeda nchini Yemen.
Mwaandishi wa Mmarekani, Luke Somers na mwalimu raia wa Afrika Kusini, Pierre Korkie wameuwawa na
wapiganaji wa Al-Qaeda nchini Yemen katika juhudi za kuwaokoa.
Oparesheni hiyo ya kuwaokoa iliongozwa na vikosi maaulum vya Marekani na Yemen katika jimbo la kusini la Shabwa.

Mwalimu raia wa Afrika Kusini Pierre Korkie (kulia).
Rais wa Marekani Barack Obama amelaani mauaji ya kinyama ya mateka hao wawili.
Walikua wanazuiliwa na wapiganaji wa kundi la Al-Qaeda katika Bara arabu ambalo Marekani inalichukulia kuwa mojawapo wa matawi hatari duniani ya kundi kuu la al-Qaeda.

Shirika ambalo mwalimu huyo raia wa Afrika Kusini Pierre Korkie alikuwa akilifanyia kazi lilisema kuwa mateka huyo angeachiliwa leo jumapili kufuatia maafikiano ya kulipa fidia.
Marekani iliamrisha kuchukuliwa jitihada hizo kwa kuwa iliamini kwamba maisha ya bwana Somers yalikuwa hatarini.
(CHANZO: BBC SWAHILI)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa