Ijumaa, 5 Desemba 2014

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2015 , CCM YAANZA KUWEKA MAKATIBU WENYE UWEZO ZAIDI LUDEWA NA IRINGA VIJIJINI WAPANGULIWA MMOJA ANGOMA KUKABIDHI OFISI


TETESI ZA LEO:


 Katibu  wa CCM wilaya ya  Iringa  vijijini Amina Imbo kushoto akiwa na  mwenyekiti  wa UWT  Iringa vijijini Shakra  Kiwanga
Katibu mpya  wa CCM wilaya ya  Ludewa  Lusian Mbosa  akisalimiana na Rais Dkt  Jakaya  Kikwete 
Makamu  mwenyekiti  wa CCM Bara Bw  Mangula akiwa na viongozi  wa CCM 
KATIKA  kile  kinachoonyesha  ni  kujipanga  kwa ajili ya  safari ya  kuelekea  uchaguzi mkuu mwaka 2015 chama  cha mapinduzi (CCM)  kimeanza pangua  pangua  ya makatibu  wa  wilaya na mikoa  ili  kukiwezesha chama  hicho kuvuka kwa  ushindi  mwakani.

Habari  za ndani  za  chama  hicho  kutoka wilaya ya Iringa  vijijini na Ludewa zimeeleza  kuwa tayari  uongozi wa chama ngazi ya  juu  umefanya mabadiliko ya makatibu  wa  wilaya  hizo  mbili  katika  mkoa  wa Iringa na Njombe pia  mkoani Katavi  na Mbeya na baadhi ya wilaya  hapa nchini .

Mbali ya kujipanga  kwa  uchaguzi  mkuu  ila  bado habari  za ndani  zinaonyesha  kuwa kuondolewa kwa makatibu hao katika vituo  vyao imetokana na uwezo  wao  wa  kiutendaji pamoja na kutoelewana na makatibu na mwenyeviti wa CCM ngazi  za  kata .

Hata  hivyo  kwa  upande  wa  wilaya ya  Iringa  vijijini katibu  wake Bi Amina Imbo habari za  kuhamishwa  zilivuja mapema mwezi  Novemba mwaka  huu na  kuwa alipaswa  kuhamishiwa Kigoma  na nafasi yake Iringa  ilidaiwa  kuchukuliwa na Roda George  ila baadae  suala  hilo  lilikwama baada ya baadhi ya  viongozi kuingilia kati na  kupigania uhamisho  huo  kusitishwa .

Kutokana na vigogo  kuingilia kati  baadhi ya makatibu kata  walianza  kampeni  za  chini kwa  chini kupinga katibu huyo kuendelea  kuwepo kwa madai kuwa hana  ushirikiano mzuri na wao  hivyo ni  heri CCM Taifa  ilivyoamua  kumbadilisha .

Taarifa  zilizoufikia mtandao  huu wa matukiodaima leo  na  kuthibitishwa na baadhi ya  viongozi  wa CCM zinadai kuwa tayari  katibu  mpya  wa  wilaya ya  Iringa  vijijini amefika  ofisini na kuripoti kwa ajili ya kuanza kazi na kuwa katibu  huyo Mahida  Mbogo ametokea  wilaya ya Mpanda japo  hadi  sasa aliyekuwa katibu  wa wilaya  hiyo ya Iringa vijijini Amina Imbo haifahamiki ni  wilaya gani atakwenda .

Huku katika wilaya ya Ludewa  Eliud  Shemauya  habari  kutoka kwa makatibu  wake wa kata  zinadai kuwa kuhamishwa  kwake ni kutokana na kutokuwa mkweli na muwazi katika mambo yake na hata  ushirikiano na makatibu na  wenyeviti  ulionekana  kuwa wa  chini  zaidi.

Kwa  sasa katibu  mpya  wa  wilaya  ya  Ludewa ambae  tayari  ameripoti ni Bw Luciana Mbosa huku taarifa  zikidai kuwa kuna uwezekano  wa  katibu  huyo kuendelea  kuwepo  hadi  upite  uchaguzi wa  serikali  za  mitaa.


Pia  katika  wilaya ya  Makete  tetesi  zinadai  kuwa katibu  wa  CCM wilaya  hiyo  ni  miongoni mwa  makatibu  waliokumbwa na pangua pangua  hiyo na chanzo  cha  kupanguliwa ni  kuwa tofauti na mbunge wa  jimbo  hilo Dr Binilith Mahenge na  kumuunga mkono mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo Bw  Okoka Sanga .

                         Hizi  ndizo   tetesi  za  leo  wadau zinafuatiliwa  zaidi  kupata ukweli  wa  tetesi   hizo 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa