Jumapili, 7 Desemba 2014

MASHINDANO YA MICHEZO YA WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI YAANZA JIJINI ARUSHA

SAM_0436
Maandamano ya mashindano ya michezo ya wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC),jijini Arusha ambayo yanatimua vumbi Uwanja Sheikh Amri Abeid  jijini Arusha kwanzia tarehe 6 hadi 12 mwezi huu
SAM_0464
Wabunge wa bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania wakifwatilia ufunguzi rasmi wa bonanza la mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kulia ni kiongozi wa timu ya bunge la Tanzania Idd Azan katikati ni Mh.mbunge Stevin Ngonyani a.k.a Maji marefu
SAM_0493
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akifurahia ushindi baada ya kushinda nafasi ya kwanza kupeperusha vema bendera ya Tanzania baada ya kuibuka mshindi  mbio za mita 100 akifuatiwa na Isaac Melley wa Kenya na Tom Aza wa Uganda aliyeshika nafasi ya tatu.
SAM_0514
Wabunge wa Tanzania Halima Mdee na Ester Matiko waliendeleza ubabe wa bunge la Tanzania dhidi ya wenzao baada ya kushika nafasi ya kwanza na pili katika mbio za mita 1,500 na kuwaacha wenzao kutoka Uganda, Kiiza Winfred na Kangi Elizabeth wakishikilia nafasi za tatu na nne.
SAM_0498
Mbunge Ester Matiko wa Tanzania  akijiandaa kukimbia mbio za mita 400,ambapo aliwatimulia vumbi wabunge wenzake kutoka Kenya, Uganda na bunge la Afrika Mashariki (Eala).
SAM_0469
Kaimu Spika wa bunge la EALA Chris Opoka akizungumza katika ufunguzi wa mashindano hayo
SAM_0470
Mkuu wa wilaya Arumeru Mhe Nyirembe Munasa afungua mashindano ya michezo kwa wabunge ambapo aliwataka wachezaji kuacha kuamini imani za kishirikina na badala yake wamtegemee Mungu kwani michezo ni kazi kama ajira nyingine
SAM_0440SAM_0452
SAM_0495
Mkurugenzi wa KeyMedia Agency Limited Bi Anna Lazaro akiwa na wabunge wa Tanzania leo jijini Arusha katika mashindano ya michezo mbalimbali yaliyoandaliwa na EALA(East African Legislative Assembly)
SAM_0508
Katikati Mkurugenzi wa KeyMedia Agency Limited Bi Barbra Lazaro akiwa na wabunge wa Tanzania leo jijini Arusha katika mashindano ya michezo mbalimbali yaliyoandaliwa na EALA(East African Legislative Assembly)
SAM_0559
Aliyevalia t-shart ya njano ni designer mkuu wa kampuni ya KeyMedia Agency Limited Bahati Masawe akiwa na waheshimiwa Wabunge
SAM_0553
Mbunge wa EALA kutoka nchini Tanzania Mh.Twaha Taslama akiwa anavuta kamba wakati wa mashindano ya hayo
SAM_0489
Mbunge wa Kenya akiwa amebebwa juju baada ya kushinda katika mbio za mita 100
SAM_0494
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mkoa wa Mara, Ester Bulaya akiwa anashangilia kwa furaha katika mashindano hayo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa