Jumamosi, 6 Desemba 2014

NYOSO ATUA MBEYA CITY FC


Na EmanuelMadafa,Mbeya
Baada ya kumaliza na kufanikiwa kumrudisha kocha wake, Jumma Mwambusi aliyetishia kuondoka katika klabu hiyo kutokana na matokeo mabaya, klabu ya Mbeya City imefanikiwa kumsajili beki kisiki Jumma Nyoso.
Kabla ya kutua Mbeya City, Nyoso alikuwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na nyingine ya ligi Kuu ya Coastal Union katika msimu iliopita .
Kusajiliwa kwa beki huyo kisiki aliyewahi kutamba na timu za Simba na Taifa stars, huenda ikasaidia kuiokoa timu hiyo na matokeo mabaya iliyoyapata tangu kuanza kwa ligi kuu ya Tanzania Bara, Septemba 20 mwaka huu.
Katika michezo saba iliyocheza kabla ya ligi kusimama imefanikiwa kushinda mchezo mmoja tu na sare michezo miwili, huku ikifungwa michezo minne.
Hali hiyo ilionekana kuwakera mashabiki wa timu hiyo ambayo msimu uliopita ilipata mafanikio makubwa na kufanikiwa kumaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa